Breaking News
recent

MAMBO USIYOYAJUA KUHUSU MAREHEMU PAUL WALKER.

    Kwa mashabiki wa movie za FAST & FURIOUS likuwa huzuni kubwa pale mwigizaji Paul walker alipofariki dunia katika ajali  ya gari.Yafuatayo ni baadhi ya mambo ambayo inawezekana ulikuwa huyajui  mwigizaji Paul Walker.                         

  1.paul Walker alikuwa anapenda sana kuendesha magari kwa kasi na mara kadhaa amewahi   kushiriki mashindano ya magari "Redtime racing series" akitumia gari yake aina ya BMW.                                                        

 2.Paul walker alikuwa ana moyo wa kusaidia watu alianzisha mfuko uitwao"Reach    Worldwide" uliokuwa unalenga kutoa msaada kwa nchi zilizokumbwa na majanga asili.Pia  Paul Walker aliwahi kumsaidia Veterani mmoja wa kijeshi aliyekuwa dukani akitafuta pete ya  ndoa kwa aajili ya mke wake.Paul alimwambia muuza duka kuwa yeye ndiye atakayelipa  bili  ya veterani huyo.

                      

 3.Paul Walker alikuwa rafiki mkubwa sana kwa waigizaji wenzake Vin Diesel Na Tyrese Na    walikuwa wakimuita Paul jina la utani "Pablo".                                                     

  4.Paul walker alikuwa ana mkanda wa brown wa sanaa ya mapigano ya kibrazili iitwayo "ji    jitsu" na alikuwa anakaribia kupewa mkanda mweusi kabla hajafa hivyo siku ya mazishi yake  mwalimu wake aliuweka mkanda mweusi juu ya jeneza kama ishara ya heshima na kumbu    kumbu.                     

 5.Paul Walker aliaanza kuonekana katika televisheni tangu akiwa mdogo mnamo miaka ya      70's Paul Walker alionekana katika tangazo la  la kutangaza Pampers.                    

6.Mke wa  Vin Diesel alipojifungua mtoto wa kike mtoto huyo alipewa jina la "Pauline"  Vin  Diesel alimpa mwanae jina hilo kama ishara ya kumkumbuka na kumuenzi rafiki yake Paul  Walker.                                

7.Paul Walker aliigiza movie yake ya kwanza mwaka 1985 wakati huo paul walker alikuwa na    umri wa miaka kumi tu.Movie hiyo ilikuwa inaitwa MONSTERS IN THE CLOSET.


No comments:

Powered by Blogger.