Breaking News
recent

MJUE LENKA (ASIYEVUMA LAKINI YUMO).

  

Ilikuwa mwaka 2010 wakati huo nilikuwa Form 2' nakumbuka nilikuwa natumia simu flani ya Tecno mchina Niliingia zangu WAPTRICK nikaingia kwenye option ya "most downloaded" ndipo nikakuta nyimbo ya mdada huyu "Lenka Kripac" kutoka Australia' niliikuta nyimbo yake inayoitwa "everythin at once" nikai-download ndipo nilipoanza kumkubali na kuukubali mziki wake Na nikawa mmoja wa shabiki wake mkubwa' Lenka sio maarufu sana kama Rihanna' Beyonce' Nick Minaj' Ariana Glande' Taylor swift au Katty Perry' Hata katika mitandao ya kijamii Lenka hana mashabiki wengi' kwa mfano katika instagram Lenka hajafikisha followers hata 10 k' Lakini hiyo haimaanish kuwa Lenka hajui muziki ANAJUA tena sana' Lenka ni Mwimbaji na pia mwigizaji Alionekana katika movie ya THE LOST THINGS na pia nyimbo zake zilitumika kama sound-track katika movie ya THE PANIC ROOM' Album yake ya kwanza Lenka aliitoa mwaka 2008 ilikuwa inaitwa 'THE SHOW" na ikashika namba 142 katika "BILLBOARD 200" nyimbo yake ya "everything at once" ilitumika kwenye kutangaza, WINDOWS 8. Na pia ilitumika katika matangazo ya movie za Disney.Lenka anasifika kwa upekee wa video zake anatengenezewa na James Guillveer Hancock ambaye ni prodyuza na mumu wake pia.Humjui Lenka? anza kumsikiliza leo.


No comments:

Powered by Blogger.